SAJENTI TAABAN, MATUMAINI BADO HANA MATUMAINI

 Tumaini Mwakibibi ‘Matumaini’ akiwa amelazwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja, Dar.
SAJENTI
Habari zisizokuwa na shaka zilizotua kwenye dawati la Ijumaa Wikienda, wikiendi iliyopita zilieleza kuwa Sajenti alizidiwa ghafla akiwa nyumbani kwake ambapo Ijumaa iliyopita alikimbizwa katika Hospitali ya Kinondoni kwa Dokta Mvungi, Dar akiwa hoi kwa ajili ya vipimo na matibabu.
Ijumaa Wikienda lilifika hospitalini hapo na kumkuta msanii huyo akiwa katundikiwa ‘dripu’ ambapo kwa mujibu wa data za ndani, vipimo vilionesha kuwa alikutwa na malaria na homa ya matumbo hivyo kumfanya aishiwe nguvu.
Hadi gazeti hili linakwenda mtamboni, Sajenti alikuwa hajaruhusiwa kutoka hospitalini.
MATUMAINI
Wakati Sajenti akiombewa na wasanii wenzake arejee katika hali yake ya kawaida, kwa upande wake Matumaini alikuwa akiendelea kupatiwa matibabu baada ya kugunduliwa kuwa na tatizo la figo, ini na miguu kuwaka moto.
Naye hali yake bado siyo nzuri tangu aliporejeshwa nchini akitokea Msumbiji akiwa taaban wiki mbili zilizopita.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment