Kundi la wanamgambo wa
kiisilamu nchini Somalia, al-Shabab wameweza kufungua ukurasa mpya wa
Twitter kwa lugha ya kiingereza, ikiwa chini ya wiki mbili tangu ukurasa
wao wa zamani kufungwa.
Afisaa mmoja mkuu wa kundi hilo, aliambia BBC kuwa ukurasa huu mpya ni halali.Sheria za mtandao wa kijamii wa Twitter zinasema kuwa ujumbe wa vitisho kuhusu ghasia umeharamishwa , ingawa kampuni ilikataa kutoa tamko lolote kuhusu kitendo cha kufunga ukurasa huo.
Ukurasa mpya wa al-Shabab una watu 280 wanaofuatilia kundi hilo kwa karibu ikilinganishwa na ukurasa wake wa awali uliokuwa watu 20,000 waliowafuatilia.
Ulifungwa tarehe 25 mwezi Januari, wiki moja baada ya kutangaza mauaji ya jasusi wa Ufaransa Denis Allex, ambaye walikuwa wamemzuilia.
Wadadisi wanasema kuwa Marekani ilitaka al-Shabab kupigwa marufuku kutumia mtandao wa Twitter, ingawa haikufanikiwa kwa sababu za kisheria.
Al-Shabaab wamefurushwa kutoka miji mikubwa ya Somalia katika kipindi cha miezi 18 ingawa bado inadhibiti maeneo ya Kusini mwa Somalia.
0 comments:
Post a Comment