ALIYEMUUA OSAMA AFUNGUKA

RISASI tatu zilimmaliza Osama bin Laden na kuandika historia.Karibu miaka miwili sasa, baada ya kimya na siri ya namna mauaji hayo yalivyofanyika, siri iliyofichwa imewekwa wazi kuhusu namna Osama alivyowapa kiwewe askari waliomvamia nyumbani kwake ambao walishindwa kumkamata akiwa hai tofauti na dhamira ya awali.

Askari aliyetekeleza mauaji hayo, tayari amefunguka na kueleza kwamba mshtuko alioupata alipokutana uso kwa uso na kiongozi huyo ulimsukuma kutekeleza mauaji yake.

“Nilimpiga risasi tatu. Nilimshuhudia akiwa amekufa ulimi nje. Nilimwona namna alivyokuwa akikata pumzi yake ya mwisho. Niliuliza akilini: Hivi hili ni jambo jema au ni jambo baya kabisa kuwahi kulifanya katika maisha yangu?”anaeleza askari huyo.

Askari huyo ambaye alipewa jina la the Shooter “mdunguaji” amesema hawakuwa na uhakika wa kumshinda, hadi walipofanikiwa kumtia nguvuni akiwa chumbani kwake katika uvamizi uliofanyika usiku wa manane.

Operesheni hiyo ilifanyika Mei 2, 2011 baada ya maandalizi yaliyowawezesha askari sita wa Marekani kumvamia kiongozi huyo wa kikundi la Al Qaeda aliyekuwa akisakwa kwa gharama zote na Marekani akiwa katika makazi yake huko Jalallabbad, Pakistan.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment