BABY MADAHA ANASWA NA BWANA WA WEMA

Baby Joseph Madaha.
Gladness Mallya na Hamida Hassan
MSANII wa filamu na muziki Bongo, Baby Joseph Madaha hivi karibuni alinaswa nyumbani kwa kigogo anayetoka na Wema, Clement.
Kwa mujibu wa chanzo kilichoomba hifadhi ya jina lake, tukio hilo lilitokea hivi karibuni ambapo staa huyo wa filamu na muziki alionekana akiingia kwa usafiri wa teksi nyumbani kwa kigogo huyo anayeishi maeneo ya Mwananyamala-Gereji, Dar.
Baada ya kujiridhisha na maelezo ya sosi huyo, mapaparazi wetu walimtafuta Baby Madaha ili kujua ukweli wa jambo hilo.
“Kweli nilikwenda hapo (kwa Clement), mimi sijui kama niliyeenda kuonana naye ni bwana wa Wema kwa sababu sijawahi kumuona naye na nilimfuata kwa ajili ya kuzungumza mambo ya kikazi,” alisema Baby Madaha.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment